Maombi haya nilipata kuomba wakati naombea ndoa na watoto,ni vizuri tukishirikishana pia pamoja.
Katika ndoa
1.Kuomba Mungu atuinue katika ndoa kwenda kiwango kingine(katika ulinzi,hekima nk.) kadiri anavyotuinua katika maeneo mengine ya maisha.(utukufu hadi utukufu)
2.Kuomba kuwa na moyo wa shukrani na wenye kuridhika(grateful and appreciative heart)
Kwa watoto
1.Kuombea character development ya watoto,Mungu aondoe visivyofaa vyote.Hapa ni vizuri tukiombea:
-Kuondoa watu wasio sahihi katika maisha na makuzi yao na kujiunganisha na watu sahihi watakaolea kusudi la Mungu ndani yao
-Kuomba walindwe na uovu na uasi na kila pando asilolipanda Mungu lingolewe ndani yao
-Kusema na nafsi zao kwa kuwataja majina kuwa ziukatae uovu na kukubali lililo jema katika ufahamu na mioyo yao;wapende haki na wadumu katika upendo
-Kupanda Neno la Mungu ndani yao kwa kuwatamkia katika maombi mistari ya Neno la Mungu mfano Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako,kwa roho yako,akili yako na kwa nguvu zako zote
-Kuomba Mungu afunulie wazazi tuweze kujua wito na karama za Mungu ndani ya watoto wetu ili tushirikiane na Mungu katika kuwepeleka mahali sahihi kukuza na kuimarisha karama zao na makusudi ya Mungu yakathibitike kwa wakati wake katika maisha yao.
Note:
Wakati naombea hivyo nikapata kutafakari kuwa matatizo mbalimbali tunayoyapata mfano changamoto za wasaidizi wa ndani ni kwa sababu hatuombei ndoa zetu na watoto wetu kwa kina kwani tukiombea maeneo hayo kwa kina Mungu ataleta watu sahihi na wala sio wa kuleta uharibifu.
Mimi nimejifunza kitu kweli hapo katika tafakari maaana nilikuwa tu naomba nipate mtu mzuri wa kunisaidia kazi kumbe nilipaswa kupanua wigo wa maombi yangu kuombea kwa kina ndoa na watoto pia.
Mungu Mwema na atubariki sote.
Friday, May 22, 2015
Subscribe to:
Comments (Atom)