Twakusihi Mungu kwa huruma yako ee Mungu, tuwezeshe kujitoa kwako
kuwa sadaka hai, takatifu na inayokupendeza Mungu, ambayo ndio ibada yetu ya
kiroho. Wala
tusiige tabia na mienendo ya dunia hii bali tubadilishwe, nia zenu zifanywe
kuwa mpya, ili tupate kuwa na hakika ni nini mapenzi yako Mungu: yaliyo mema,
yanayopendeza machoni pako na makamilifu. Rum 12:1-2
Utujalie ee Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu,roho
ya hekima na ya mafunuo tupate kukufahamu zaidi. macho ya mioyo yetu yaangaziwe ili tupate kujua tumaini tuliloitiwa, na
tutambue utajiri wa urithi wa utukufu wake kwa watu wa Mungu; na tuu fahamu
uweza wake usiopimika ambao ametupa sisi tunaoamini. Uweza huo ni sawa na ile
nguvu kuu ambayo
uliitumia ulipomfufua Kristo kutoka kwa wafu, ukamweka akae mkono wako wa kulia
katika enzi yako mbinguni. Hapo
alipo ni juu sana, kupita tawala na mamlaka zote na nguvu zote na milki, na
kupita cheo cho chote kinachoweza kutolewa, si tu katika nyakati hizi, bali pia
katika nyakati zijazo. Nawe
Mungu umeweka vitu vyote viwe chini ya mamlaka yake na ukamteuwa awe mkuu wa
vitu vyote kwa ajili ya kanisa, ambalo
ni mwili wake, nalo limejawa na yeye ambaye hujaza kila kitu kwa kila njia.
Tumefanywa Kuwa Hai Ndani Ya Kristo. Efe 1:17-23
Na
kupitia katika hiyo neema na utume
tuliokirimiwa na wewe Mungu kwa njia ya Yesu kristo Tupate kuyaweza yote mambo yote katika wewe ututiaye
nguvu. Rum 1,Fil 4