God Graciously hear us

May your angles Lord be constantly bringing these prayers before you

Grant Us your Peace always for you said in Phil 4:4-7

4Rejoice in the Lord always. I will say it again: Rejoice! 5Let your gentleness be evident to all. The Lord is near. 6Do not be anxious about anything, but in everything, by prayer and petition, with thanksgiving, present your requests to God. 7And the peace of God, which transcends all understanding, will guard your hearts and your minds in Christ Jesus.

Friday, April 20, 2018

Utuinue na kutuimarishe ee Bwana

Utuinue na kutuimarishe ee Bwana sisi Kanisa lako

Twakusihi Mungu kwa huruma yako ee Mungu, tuwezeshe kujitoa kwako kuwa sadaka hai, takatifu na inayokupendeza Mungu, ambayo ndio ibada yetu ya kiroho. Wala tusiige tabia na mienendo ya dunia hii bali tubadilishwe, nia zenu zifanywe kuwa mpya, ili tupate kuwa na hakika ni nini mapenzi yako Mungu: yaliyo mema, yanayopendeza machoni pako na makamilifu. Rum 12:1-2

Utujalie ee Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu,roho ya hekima na ya mafunuo tupate kukufahamu zaidi.  macho ya mioyo yetu yaangaziwe ili tupate kujua tumaini tuliloitiwa, na tutambue utajiri wa urithi wa utukufu wake kwa watu wa Mungu;  na tuu fahamu uweza wake usiopimika ambao ametupa sisi tunaoamini. Uweza huo ni sawa na ile nguvu kuu  ambayo uliitumia ulipomfufua Kristo kutoka kwa wafu, ukamweka akae mkono wako wa kulia katika enzi yako mbinguni.  Hapo alipo ni juu sana, kupita tawala na mamlaka zote na nguvu zote na milki, na kupita cheo cho chote kinachoweza kutolewa, si tu katika nyakati hizi, bali pia katika nyakati zijazo. Nawe Mungu umeweka vitu vyote viwe chini ya mamlaka yake na ukamteuwa awe mkuu wa vitu vyote kwa ajili ya kanisa,  ambalo ni mwili wake, nalo limejawa na yeye ambaye hujaza kila kitu kwa kila njia. Tumefanywa Kuwa Hai Ndani Ya Kristo. Efe 1:17-23


Na kupitia katika hiyo  neema na utume tuliokirimiwa na wewe Mungu kwa njia ya Yesu kristo Tupate  kuyaweza yote mambo yote katika wewe ututiaye nguvu. Rum 1,Fil 4


Wednesday, September 20, 2017

Uturudishe Ee Bwana



Ututakase ee Bwana,kanisa lako la Tanzania,kama ulivyoahidi

24 Maana nitawatwaa kati ya mataifa, nami nitawakusanya na kuwatoa katika nchi zote, na kuwarudisha katika nchi yenu wenyewe.
25 Nami nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi; nitawatakaseni na uchafu wenu wote, na vinyago vyenu vyote.
26 Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama.
27 Nami nitatia roho yangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu, nanyi mtazishika hukumu zangu, na kuzitenda.
28 Nanyi mtakaa katika nchi ile niliyowapa baba zenu, nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.
29 Nami nitawaokoeni na uchafu wenu wote; nitaiita ngano, na kuiongeza, wala sitaweka njaa juu yenu tena.
30 Nami nitazidisha matunda ya miti, na mazao ya mashamba, msipate tena kutukanwa na mataifa kwa sababu ya njaa.
31 Ndipo mtazikumbuka njia zenu mbaya, na matendo yenu yasiyokuwa mema, nanyi mtajichukia nafsi zenu kwa macho yenu, kwa sababu ya maovu yenu na machukizo yenu.

32 Ijulikane kwenu ya kuwa silitendi neno hili kwa ajili yenu, asema Bwana MUNGU; tahayarikeni, na kufadhaika, kwa sababu ya njia zenu, Enyi nyumba ya Israeli.


Wednesday, September 13, 2017

Kuomba kuimarishwa

15  Mungu tunaomba utujalie kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wako, kufanywa imara kwa nguvu, kwa kazi ya Roho wako katika utu wa ndani. 
16  Kristo akae mioyoni mwetu kwa imani tukiwa na shina na msingi katika upendo; 
17  ili tupate kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, na urefu, na kimo, na kina; 
18  na kuujua upendo wako Kristo, upitao ufahamu kwa jinsi ulivyo mwingi, tupate kutimilika kwa utimilifu wote wa Mungu. 
19  Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu; 
20  naam, atukuzwe katika Kanisa na katika Kristo Yesu hata vizazi vyote vya milele na milele. Amina.  Efe 3:15-20

Monday, September 28, 2015

Unitakase na unilinde Ee Bwana,kiburi kisinitawale

Ee Mungu,Ni nani awezaye kuyatambua makosa yake? Unitakase na mambo ya siri.
Umzuie mtumishi wako asitende mambo ya kiburi, Yasinitawale mimi. Ndipo nitakapokuwa kamili, Nami nitakuwa safi, sina kosa lililo kubwa.
Maneno ya kinywa changu, Na mawazo ya moyo wangu, Yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu, na mwokozi wangu. Zab 19:7-14

Thursday, September 10, 2015

Yesu Mfalme wangu,ufalme wako uje ndani yangu.

Mungu baba naomba unisamehe kwa kuruhusu wakati wowote kiti cha enzi cha uovu/shetani kuingia ndani yangu kwa kujua au kutokujua,ninaomba unitakase kwa damu yako Yesu na ninakivunja hicho kiti,ninakipindua na kukukaribisha Yesu uingie kuchukua nafasi ya utawala katika maisha yangu.Njoo ufanyike mfalme wangu,mwamuzi wangu na mtunga sheria wangu.Ee Yesu ufalme wako uje,haki yako ifanye makao yake daima ndani yangu niweze kumiliki na kutawala pamoja nawe Yesu

Katika Jina la Yesu nakataa kila ushirika na ulimwengu wa giza na mikataba na maagano yote niliyoingia nayo naivunja na kubatilisha kwa Jina la Yesu,Napokea agano la Damu ya Yesu katika maisha yangu kama agano kuu lenye kusimamia maisha yangu,Asante Yesu kwa Kunikomboa na kunipatanisha na Mungu na kunifanya mwenye haki wa Mungu.Uhimidiwe Mungu Mkuu unayestahili kusifiwa na kuadhimishwa milele.


Friday, May 22, 2015

Prayer Points

Maombi haya nilipata kuomba wakati naombea ndoa na watoto,ni vizuri tukishirikishana pia pamoja.

 Katika ndoa
1.Kuomba Mungu atuinue katika ndoa kwenda kiwango kingine(katika ulinzi,hekima nk.) kadiri anavyotuinua katika maeneo mengine ya maisha.(utukufu hadi utukufu)

2.Kuomba kuwa na moyo wa shukrani na wenye kuridhika(grateful and appreciative heart)


Kwa watoto
 1.Kuombea character development ya watoto,Mungu aondoe visivyofaa vyote.Hapa ni vizuri tukiombea:
-Kuondoa watu wasio sahihi katika maisha na makuzi yao na kujiunganisha na watu sahihi watakaolea kusudi la Mungu ndani yao
-Kuomba walindwe na uovu na uasi na kila pando asilolipanda Mungu lingolewe ndani yao
-Kusema na nafsi zao kwa kuwataja majina kuwa ziukatae uovu na kukubali lililo jema katika ufahamu na mioyo yao;wapende haki na wadumu katika upendo
-Kupanda Neno la Mungu ndani yao kwa kuwatamkia katika maombi mistari ya Neno la Mungu mfano Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako,kwa roho yako,akili yako na kwa nguvu zako zote
-Kuomba Mungu afunulie wazazi tuweze kujua wito na karama za Mungu ndani ya watoto wetu ili tushirikiane na Mungu katika kuwepeleka mahali sahihi kukuza na kuimarisha karama zao na makusudi ya Mungu yakathibitike kwa wakati wake katika maisha yao.

Note: Wakati naombea hivyo nikapata kutafakari kuwa matatizo mbalimbali tunayoyapata mfano changamoto za wasaidizi wa ndani ni kwa sababu hatuombei ndoa zetu na watoto wetu kwa kina kwani tukiombea maeneo hayo kwa kina Mungu ataleta watu sahihi  na wala sio wa kuleta uharibifu.

Mimi nimejifunza kitu kweli hapo katika tafakari maaana nilikuwa tu naomba nipate mtu mzuri wa kunisaidia kazi kumbe nilipaswa kupanua wigo wa maombi yangu kuombea kwa kina ndoa na watoto pia. Mungu Mwema na atubariki sote.

Wednesday, November 6, 2013

Power to will,do and persist-overcome spiritual negligence

Ooh God,Lord Almighty,I pray that you always give me the power to will,do and persist in all that I am supposed to according to your will.

Give me the power to overcome any kind of spiritual as well as physical negligence in my life and be able to play my spiritual as well as physical positions with all the Authority from you God properly making your Name Glorified forever whilst persisting in your loving care and relation.

In Jesus Christ I pray,AMEN.